KANISA KATOLI TANGA

this page in english

St. Anthony's Cathedral
YOUNG CHRISTIAN STUDENTS(TYCS)

 

Young Catholic Students – TYCS ni kikundi cha kitume ambacho wanachama wake ni wanafunzi. Chama hiki kipo katika ngazi ya Sekondari na vyuo. TYCS inawapa mafunzo wanachama wake ushujaa wa kuangali kuchunguza mazingira ya uaanafunzi na kumtangaza Kristo katika mazingira hayo. Chama hiki pia huamsha vipaji mbalimbali vya wanachama na kuwafanya watambue vipaji vyao na kuviendeleza. Kazi hii hufanywa kwa maongozi ya Roho Mtakatifu. Pia huwapatia wanachama wake semina mbalimbali za kiroho, makongamano na mafungo yatakayowafanya watafakari zaidi neno la Mungu.

TYCS inajitokeza katika kila shule ya sekondari ambapo panawanafunzi wakristo. Kwanza uanza kama kikundi kidogo katika shule kisha ujumuisha kanda na hatimae jimbo na pia Taifa.


TYCS huleta mbele ya wanachama wake wazo kuu ambalo ni kumtangaza Kristo katika mazingira ya uanafunzi. Pia huwafundisha na kuwaonesha njia vijana wakiume na wakike kujiunga na wito wa upadre ama utawa na kuwaandaa kuwa viongozi bora popote watakapokuwa katika nchi.

Jimboni Tanga, Chama hiki kilianzishwa na marehemu Padre. Gerald Smith mwaka 1970 Chumbageni Tanga. Tangu mwaka 1976 PadreJames Kweka amakuwa masimamizi wa chama hiki cha TYCS. Mwaka 1994 Pd. Titus Mdoe amechukua jukumu hili la kukilea chama hiki na pia kama mkurugenzi wa miito mpaka mwaka 2006 pale alipokwenda masomoni Marekani. Kazi hii ya kukilea chama hiki na kushughulikia miito ilikabidhiwa kwa Pd. John Zuakulu. Chama hiki cha TYCS kipo karibu katika kila shule na vyuo hapa Jiboni Tanga. TYCS imefanya mambo mengi Jimboni Tanga, hasa kuwaleta wanafunzi pamoja, kufahamiana na kuinua vipaji vyao.

Baada ya kumaliza masomo yao, wana TYCS bado wameendelea kuwa mfano mzuri sana katika maisha kama wakristo. Wamekuwa mfano mzuri kwa wakristo wenzao.le of Christian life in their respective Churches. They participate well in all activities in the Church, for example in the choirs and other activities.